Mpaka kufikia 2021 serikali imeahidi kusambaza umeme wa kutosha na wa uhakika katika vijiji vyote nchini ili kuendana na dhamira ya kuelekea katika uchumi wa kati kupitia viwanda.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Nishati na Madini Prof. Sospeter Muhongo wakati wa kipindi cha TUNATEKELEZA kinachorushwa na Televisheni ya Taifa ya TBC1 kwa ushirikiano na Idara ya Habari-MAELEZO.

Prof. Muhongo alisema kuwa kukamilika kwa miradi ya kuzalisha nishati ya umeme ikiwemo Mradi wa Kinyerezi 1 unaozalisha megawati 150 kwa siku umesaidia kuongeza upatikanaji wa huduma ya umeme wa kutosha mijini na baadhi ya vijiji.

“serikali sasa ipo katika kutekeleza miradi mikubwa ya nishati za umeme na gesi ikiwa ni jitihada za kuhakikisha mpaka kufikia 2021 vijiji vyote nchini viwe vimepata huduma ya nishati ya umeme”. Alisema Prof. Muhongo.

Aidha, Prof. Muhongo alisema kuwa utekelezaji wa Miradi hiyo unaenda sambamba na lengo la Serikali ya awamu ya Tano ya kuwa na uchumi wa kati kupitia viwanda ifikapo 2025.

Akizungumzia kuhusu mikakati ya kuthibiti utoroshaji wa madini nchini Prof. Muhongo alisema kuwa serikali inaendelea kuweka mikakati ya kuwakamata  watoroshaji wa madini hasa katika maeneo ya mipakani na viwanja vya ndege.

Prof. Muhungo alisema kuwa kuanzia mwaka 2012 wamekamata madini ya aina mbalimbali zaidi ya Tani 10 yaliyokuwa yanatoroshwa kutoka nchini kwenda nchi mbalimbali.

Prof. Muhongo amewataka watanzania kutumia fursa mbalimbali zitakazotokana na utekelezaji wa miradi katika sekta ya gesi na mafuta ili kujiongezea kipato na kuiwezesha nchi kutimiza malengo yake kuelekea kuwa nchi ya uchumi wa kati.

Kesi Ya Simba Na Yanga Kuhusu Kessy Yaahirishwa
Rais Magufuli;Ole Wake Atakae Hatarisha Amani Ya Nchi, Asema Hatomvumilia Mtu, Aagiza Vyombo Vya Dola Kuanza Kuwashughulikia