Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa wakuu wa mikoa wapya 9 leo 28, Julai 2022.

Katika uteuzi huo waliobakia kwenye vituo vyao ni 10 na waliohamishwa ni 7.

Miongoni mwa Waliobadilishwa Mikoa ni Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Antony Mtaka na badala yake ni Rosemary Senyamule.

Miongoni mwa walioondolewa katika nafasi hiyo ni aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Marco Gaguti, aliyrkuwa Mkuu wa mkoa wa Singida Bilnith Mahenge, aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara Ally Hapi.

Uapisho utafanyika Agosti mosi Ikulu Chamwino Jijini Dodoma.

Habari kuu kwenye magazeti ya leo Julai 28, 2022
Uchumi wa Duniani wazidi kufifia