Rais wa Marekani Barack Obama ameendelea kuonesha mapenzi yake kwenye mchezo wa kikapu baada ya taarifa kutoka kwa kaimu msemaji wa ikulu ya Marekani (White House)  Josh Earnest kudai kuwa mara baada ya kumaliza muhula wake wa mwisho kama rais wa taifa hilo kubwa duniani mwaka huu,huenda Rais Obama atawekeza kwenye mchezo huo wenye mashabiki wengi nchini humo,kwa kununua moja ya klabu zinashiriki ligi kuu ya kikapu ya Marekani NBA