Neema ya uteuzi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli imemgusa Waziri Mkuu Mstaafu, Mizengo Pinda.

Rais Magufuli leo ametangaza kumteua Mizengo Pinda (mtoto wa mkulima) kuwa Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (Open University of Tanzania).

Nafasi hiyo awali ilikuwa ikishikiliwa na Balozi, Dkt. Asha Rose Migiro ambaye hivi karibuni aliteuliwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Uingereza.

 

MABULA :MIUNDOMBINU MIBOVU HUSABABISHA AJALI ZA MOTO
Waziri avunja Bodi ya TCU kwa kupitisha wanafunzi wasio na sifa kusomea Shahada