Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt.Hussein Mwinyi ametangaza ongezeko la mshahara kwa 15% kwa wafanyakazi wa Visiwani humo.

Rais Mwinyi ametangaza ongezeko hilo Leo Mei 8, katika kilele cha maadhimisho ya siku ya wafanyakazi kilichofanyika katika Viwanda vya maisara ambapo siku ya Mei Mosi hazikufanyika ili kupisha sikukuu ya Eid El Fitri.

Kutokana na utaratibu huo kima cha chini cha mshahara kitapanda kutoka Tsh. 300,000 hadi Tsh. 347,000 sawa na asilimia 15.6.

Dkt. Mwinyi amesema pia kiwano cicho cha mshahara kitaendana na kiwango cha Elimu ya kila mfanyakazi akitegemea pia kutokana na ongezeko hilo utendaji wa kazi utaongezeka.


Royal Tour yazinduliwa Dar
Siku ya mama:Mateso aliyopitia mama wa Trevor katika uchekeshaji