Wakati tetesi za kutimuliwa kwa kocha Louis Van Gaal zikizidi kuongezeka, mmoja wa makocha wanaotajwa kuwa katika listi ya kumrithi Jose Mourinho ameripotiwa kutaja timu atakayoenda kufundisha hivi karibuni.

Kwa mujibu rafiki wa karibu wa kocha huyo wa kireno, mkurugenzi wa klabu ya Inter Milan, Bedy Moratti, amesema kwamba Mourinho atakuwa kocha mpya wa Manchester United.

Mourinho jana alikutana na Raisi wa klabu ya Inter Milan Massimo Moratti kwa ajili ya chakula cha mchana jijini Milan, Italia, na katika mkutano huo dada yake Raisi wa klabu hiyo ya zamani ya Mourinho, Bedy Moratti pia alihudhuria.

Wakati akiwa anatoka katika mgahawa walipokutana na Mourinho – Bedy Moratti aliulizwa na waandishi wa habari kama Mourinho atarejea Inter, akajibu: ‘Nammisi kama rafiki, ni mtu mzuri sana, lakini kwa sasa ana furaha anaenda Manchester.’

Himid Mao Kuikosa Tanzania Prisons J’5
Sanchez Atia Neno Kuelekea Game Ya Arsenal Vs Barcelona