Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo amepiga marufuku kwa viongozi wa Serikali kuwakamata watumishi wa umma na kuwaweka rumande bila kufuata sheria na taratibu za utumishi wa umma.

Amesema kuwa siku za hivi karibuni kumejitokeza tabia ya baadhi ya viongozi kuwakamata na kuwaweka rumande watendaji wa serikali bila kufuata sheria na taratibu za utumishi wa umma.

“Kama mtendaji alikosea kuna taratibu za kufuata, kuna masuala ya kiutumishi, kuna masuala ya kijinai na kiuchunguzi hivyo ni vyema yakafuatwa, lakini si kukurupuka tu na kuwaweka rumande,”amesema Gambo

Aidha, Gambo amewataka viongozi kutumia vyombo vilivyowekwa na serikali kutatua matatizo ikiwemo Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) pia kufuata sheria za utumishi wa umma.

Bulyanhulu kukwepa zigo la makinikia
Liverpool, Tottenham zashindwa kutamba nyumbani