Wakati chama cha Republican wakiendelea kumtetea Donald Trump, baada ya F.B.I. kufanya upekuzi katika makazi ya rais huyo wa zamani wa Marekani huko Florida, mpasuko umeonekana katika uungaji mkono wa chama kwa utekelezaji wa sheria.

Baadhi ya Wanachama wa republican wa Congress waliishambulia F.B.I. na mashirika mengine ya juu ya utekelezaji wa sheria, huku wengine wakiwapinga wenzao na na kuwatetea wanausalama hao wa F.B.I.

Agosti 12, 2022, Jaji wa shirikisho alibatilisha hati ya kuidhinisha utafutaji na orodha ya vitu vilivyoondolewa kutoka nyumbani kwa Trump na maajenti wa shirikisho hilo la F.B.I, ambapo imeonekana walipata seti 11 za hati zilizoainishwa kama sehemu ya uchunguzi kuhusu uwezekano wa ukiukaji wa Sheria ya Ujasusi na sheria nyingine mbili.

Warepublikan wengi, wametaka kuachiliwa kwa hati ya kiapo inayounga mkono hati ya upekuzi, ambayo ingefichua kile kilichomshawishi jaji kuwa kulikuwa na sababu zinazowezekana kuamini kuwa upekuzi ungepata ushahidi wa uhalifu.

Hati kama hizo kwa kawaida hazitangazwi hadharani kabla ya mashtaka kuwasilishwa, na imeripotiwa kuwa mtu mwenye bunduki aliwashambulia F.B.I. ofisini huko Cincinnati, na Ijumaa Idara ya Usalama wa Nchi ilionya juu ya “ongezeko la vitisho na vitendo vya jeuri” dhidi ya watekelezaji sheria.

Moto Kanisani: UN yatuma salamu za rambirambi
Moto Kanisani: 41 wadaiwa kufariki, Rais azungumza