Baada ya taarifa za kifo cha Mzee Majuto August 8, 2018  usiku wa kuamkia leo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili baadhi ya watu maarufu wameonyesha kuguswa na msiba huo kupitia kurusa zao za instagram.

Mbunge wa Chalinze, Ridhiwan Kikwete kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika kuwa;

“Mzee Amri Athumani Baba, Rafiki na Mzee wangu Nakushukuru kwa Maisha Uliyoyaishi. MWENYEZI MUNGU Ana sababu katika Kuonyesha Upendo wake. Tunakushukuru kwa Kizazi Chako Pia…Alhaj Amri Majuto. Salamu za Pole ziende kwa Katibu Tawala Wangu wa Bagamoyo Ndg. Hamza Athumani na Nduguze wote. Tuko pamoja sana. Pumzika kwa Amani Baba Majuto”

Pia Idris Sultan ameandika kuwa; “Kazi yangu ya mwisho kama photographer/graphic designer kabla ya kwenda BBA na ndo ilikuwa mara ya kwanza kukutana na King Majuto. Mara nyingi alikuwa haji anaagiza watu wanatuma picha ila hii alikuja.”

“Nakumbuka mzee aliniambia “We dogo una vituko sana ila kituko chako kikubwa kuliko vyote ni haujui unafurahisha kiasi gani, endelea kutokujua utashangazwa”… Sidhani kama mnajua kiasi gani unajiskia ukiambiwa kitu kama hicho na mfalme. To this day nasikitika kuwa sikuwahi kumuambia alichonifanya ila naweza kumuahidi kuwa popote nitakapoenda nitahakikisha sifanyi kosa la kutokusema makubwa aliyotufanyia kama watoto wake kwenye comedy industry. FOREVER A KING ?? inna lillahi. With respect I will never call myself KING na naomba isitokee nikaitwa pia ??????”

 

 

“Muda umefika Baba Safiri Salama Kikubwa umeacha Alama kubwa kwenye Dunia na tasnia kwa ujumla Heshima yako itabaki milele PUMZIKA KWA AMANI”  -Zamaradi Mketema

 

Naye muigizaji Wema Sepetu katika ukurasa wake wa Instagram ameandika kuwa;Alipangalo Allah… I wished to work with you baba angu… Ila Allah hakupanga… Kapumzike baba angu… Mungu Mkali jamani….???… Ila kama kuteseka tu umeteseka jamani…. RIP King…”

JPM atuma salamu za rambirambi kufuatia kifo cha 'King Majuto'
Kepa Arrizabalaga avunja rekodi ya Alisson Becker