Rufaa iliyokatwa na Rais wa Shirikisho la soka duniani FIFA Sepp Blatter na Michel Platini ya kupinga kifungo cha soka cha siku 90 imekataliwa.

Adhabu hiyo ilitolewa mwezi Oktoba mwaka huu na kamati ya maadili ya shirikisho hilo.

Blatter,Valcke na rais wa UEFA Platini walisimamishwa na kamati hiyo ili kupisha uchunguzi kuhusu madai ya ufisadi.

Watatu hao wamepigwa marufuku kushiriki katika michezo yoyote ya kandanda kwa muda huo.

Blatter anatuhumiwa kwa kutia saini kandarasi isiyokuwa na umuhimu wowote kwa FIFA mbali na kutoa malipo kwa rais wa shirikisho la UEFA Michel Platini kinyume na matakwa ya shirikisho hilo.

Kamati ya maadili pia ilianzisha uchunguzi dhidi ya Platini kuhusu malipo hayo ya Yuro milioni 2 ambayo yalifanywa miaka minane baada ya Platini kumfanyia kazi Blatter.

Wabunge wa Ukawa watishia Kufanya ‘Jambo’ Endapo Dkt Shein ataingia Bungeni na Dkt Magufuli
Kuelekea Game Ya El Classico, Ulinzi Waimarishwa Mjini Madrid