Tuzo za MTV MAMA zimetolewa usiku wa kuamkia leo jijini Johannesburg, Afika Kusini huku Tanzania ikishindwa kuchomoza na tuzo kwenye vipengele kadhaa ambavyo wasanii wake walitajwa.

Kundi la Sauti Sol la Kenya, limeitoa kimasomaso Afrika Mashariki baada ya kushinda tuzo ya kundi bora la Muziki (Best Group) ambayo ni tuzo pekee iliyokuja katika ukanda huu.

Usiku huo ulikuwa mkubwa zaidi kwa Wizkid ambaye aliibuka na tuzo mbili nzito zaidi, Msanii wa Mwaka (Artist of the Year) na Msanii Bora wa Kiume (Best Male Artist), pamoja na tuzo moja ya wimbo bora wa kushirikiana (DJ Maphorisa Feat Wizkid & Dj Buckz – Soweto Baby). Hivyo kuongoza kwa kuondoka na tuzo tatu usiku huo.

Wasanii wa Tanzania waliotajwa kuwania tuzo hizo ni pamoja na Diamond Platinumz, Ali Kiba, Raymond, kundi la Yamoto Band, Vanessa Mdee na kundi la Navy Kenzo.

Hii ni orodha kamili ya washindi wa tuzo hizo:

Best Live Act: Cassper Nyovest

Best Group:   Sauti Sol  

Best Pop/Altenative Act: Shekhinah & Kyle Deutsch

 Best Female:   Yemi Alade   

Best International Act: Drake

Best Lusophone Act: C4Pedro (Angola)

Best Francophone: Serge

Best Male:  Wizkid

Listeners Choice Awards:  Jah Prayzah    

Best Collaboration: DJ Maphorisa Feat Wizkid & Dj Buckz – Soweto Baby

Video of the Year – Nique Ma VieYoussoupha (Congo)

Best Hip Hop: Emtee

Breakthrough Act:  Tekno   

Song of the Year – My Woman (Patoranking)

Artist of the Year –   Wizkid

Makamba ahamasisha utunzaji vyanzo vya maji na mazingira
Makonda aahidi mifuko 1000 ya cement, magodoro 400 Shule ya St. Joseph Millenium