Serikali imeahidi  kuhifadhi  kumbukumbu na takwimu sahihi za urithi wa Utamaduni usioshikika kwa lengo la kuuendeleza na kuiwezesha jamii kuulinda kwa ajili ya vizazi vijavyo.

Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel alipokua akifungua warsha ya siku kumi iliyoandaliwa na  Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) kuhusu urithi wa Utamaduni Usioshikika  leo Jijini Dar es Salaam.

Aidha, Prof. Gabriel amewataka washiriki kujifunza vizuri ili baadaye waweze kusaidia  katika kuwekeza, kuibua, kutambua na kutunza urithi wa utamaduni usioshikika kwani hiyo ndio njia mojawapo  itakayowavutia watalii wengi kuja nchini  kujifunza tamaduni zetu zisizoshikika.

“Utamaduni ni nta inayowaweka watu pamoja, ni vyema mafunzo haya na utaalamu mtakayoipata izingatie kuibua fursa na kutambua tamaduni ambazo hazishikiki kwani serikali ina malengo na matumaini makubwa sana kutoka kwenu” alisema Prof. Gabriel.

Kwa upande wake Mwakilishi kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO), Mathias Luhanya amesema kuwa dhumuni la warsha ni pamoja na kuwajengea uwezo wadau wa utamaduni namna ya kuhifadhi urithi wa utamaduni usioshikika ili baadaye waweze kuorodhesha urithi huo kwani Tanzania ina bahati ya kuwa na jamii zaidi ya 120 hivyo ni matarajio kuwa urithi wa utamaduni usioshikika umesheheni ndani ya kila jamii.

Alan Pardew Amshika Pabaya Mmiliki Wa Crystal Palace
Prof. Ndalichako: Maadili ni jukumu la jamii nzima