Serikali imedhamiria kuendelea kuwalinda wananchi dhidi ya madhara yatokanayo na Matumizi ya Dawa kwa lengo la Kulinda afya ya Jamii.
Kauli hiyo imetolewa na Meneja Uhusiano wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) Bi Gaudensia Simwanza wakati wa mkutano na Waandishi wa habari leo Jijini Dar es salaam.
Akifafanua Simwanza amesema kuwa Mamlaka hiyo inao mfumo wa ufuatiliaji wa Usalama wa Dawa ambao Kitaalamu unajulikana kama (Pharmacovigince) unaojumuisha utambuzi,tathmini,uelewa na udhibiti