Msemaji wa Wakala wa Ukaguzi wa Madini Tanzania (TMAA) Bw. Yisambi Shiwa akiwaeleza waandishi wa habari jijini Dar es Salaam namna walivyoimarisha udhibiti wa shughuli za uchimbaji na biashara ya madini kwa kuongeza wakaguzi migodini na vituo vya ukaguzi kwenye maeneo mbalimbali na kuhakikisha shughuli hizo zinafanyika kwa kuzingatia uhifadhi wa mazingira. Kushoto ni Kaimu Mtendaji Mkuu wa TMAA, Bw. Gilay Shamika na kulia ni Mwanasheria Bw. Gimonge Ngutunyi