Serikali kupitia Wizara ya Nchi – Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) imesimamisha utoaji huduma katika hospitali zote za Marie Stopes Tanzania (MST).

Akizungumzia sababu za kusimamisha huduma hizo, Naibu Waziri wa Tamisemi anayeshughulikia masuala ya afya, Josephat Kandege alisema kuwa hatua hiyo imechukuliwa kutokana na hospitali hiyo kukiuka miongozo.

Hata hivyo, Kandege alisema kuwa Mganga Mkuu wa Serikali ndiye anaweza kutoa ufafanuzi zaidi wa kitaalam wa sababu za kufungiwa kwa hospitali hizo.

“Mhusika ambaye atakuwa kwenye nafasi nzuri kuweza kulizungumzia suala hili ni mganga Mkuu wa Serikali ili tuwe na taarifa sahihi ya kuutarifu umma,” Kandege anakaririwa na Mwananchi.

Awali, msemaji wa MST, Dotto Mnyadi alisema kuwa hospitali hizo zimesimamishwa kutokana na ukaguzi uliokuwa unaendelea kufanywa na Serikali.

Aliongeza kuwa mbali na ukaguzi huo, kuna ukarabati ambao ulikuwa unaendelea kwa hospitali zote za MST.

Kim K ashtushwa na jibu la Kanye West kwa Rais Museveni
Canada yaruhusu matumizi ya bangi kwa tiba