Klabu ya Corinthians wametawadhwa mabingwa wapya wa Brazil jana baada ya sare ya bao 1-1 waliyopata dhidi ya Vasco da Gama na kusaidiwa na kipigo cha mabao 4-2 walichpata Atletico Mineiro dhidi ya Sao Paulo ambacho kimewafanya kuongoza kwa alama 12 huku zikiw zimesalia mechi tatu. 

Corinthians ndio vinara wa mabao katika ligi na safu imara ya ulinzi huku pia wakiwa wameshinda mechi nyingi zaidi na kufungwa chache kuliko timu nyingine yeyote. 

Klabu hiyo hiyo imenyakuwa taji hilo ambalo ni la sita kwao wakiwa wanaongoza kwa alama 77 wakati Atletico waliokuwa wakifuatia wakiwa na alama 65. 

Akihojiwa golikipa wa Corinthians aliwapongeza wachezaji wenzake kwa jinsi walivyojituma na kuongeza kuwa walistahili taji hilo.

Jean-Claude Van Damme Avamia Mazoezi Ya Man City
Dirisha Dogo La Usajili Kufungwa Disemba 15