Spika wa Bunge la Jamhuri ya muungano wa Tanzania, Job Ndugai amepokea taarifa za Kamati Maalum ya Kuchunguza Biashara ya Tanzanite na Almasi na kumkabidhi Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ambapo leo Septemba 7, 2017 itawasilishwa kwa Rais, Dkt. John Pombe Magufuli.

IMGL2724

Spika wa Bunge, Job Ndugai akimkabidhi Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa Taarifa za Kamati Maalum ya Kuchunguza Biashara ya Tanzanite na Almasi  katika tukio lililofanyika leo katika Viwanja vya Bunge Mjini Dodoma.

IMG_3215

Spika wa Bunge, Job Ndugai (kushoto) akikabidhiwa Taarifa ya Kamati Maalum ya Kuchunguza Biashara ya Almasi na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Mussa Azzan Zungu (kulia) katika tukio lililofanyika leo katika Viwanja vya Bunge Mjini Dodoma. kushoto ni Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Kulia ni Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Mhe. Freeman Mbowe

IMG_3237

Spika wa Bunge, Job Ndugai (kushoto) akikabidhiwa Taarifa ya Kamati Maalum ya Kuchunguza Biashara ya Tanzanite na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Dotto Biteko (kulia) katika tukio lililofanyika leo katika Viwanja vya Bunge Mjini Dodoma. kushoto ni Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Kulia ni Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Mhe. Freeman Mbowe

IMGL2425

Mwenyekiti wa Kamati Maalum ya kuchunguza Almasi, Mussa Azzan Zungu akizungumza wakati wa uwasilishaji wa Taarifa za Kamati Maalum ya Kuchunguza Biashara ya Tanzanite na Almasi katika tukio lililofanyika leo katika Viwanja vya Bunge Mjini Dodoma.

IMGL2529

Mwenyekiti wa Kamati Maalum ya kuchunguza Tanzanite, Dotto Biteko akizungumza wakati wa uwasilishaji wa Taarifa za Kamati Maalum ya Kuchunguza Biashara ya Tanzanite na Almasi katika tukio lililofanyika leo katika Viwanja vya Bunge Mjini Dodoma.

IMGL2588

Kiongozi wa Upinzani Bunge, Freeman Mbowe akizungumza wakati wa uwasilishaji wa Taarifa za Kamati Maalum ya Kuchunguza Biashara ya Tanzanite na Almasi katika tukio lililofanyika leo katika Viwanja vya Bunge Mjini Dodoma.

IMGL2654

Spika wa Bunge, Job Ndugai akizungumza wakati wa uwasilishaji wa Taarifa za Kamati Maalum ya Kuchunguza Biashara ya Tanzanite na Almasi katika tukio lililofanyika leo katika Viwanja vya Bunge Mjini Dodoma.

IMGL2472

Naibu Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson akizungumza wakati wa uwasilishaji wa Taarifa za Kamati Maalum ya Kuchunguza Biashara ya Tanzanite na Almasi katika tukio lililofanyika leo katika Viwanja vya Bunge Mjini Dodoma.

IMGL2787

Spika wa Bunge, Job Ndugai (wa pili kulia waliokaa), Waziri Mkuu,<iframe width=”560″ height=”315″ src=”https://www.youtube.com/embed/xzj5HyM_4uM” frameborder=”0″ allowfullscreen></iframe> Kassim Majaliwa (wa pili kushoto waliokaa), Naibu Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson (kushoto waliokaa) na Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe (kulia waliokaa) wakiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Kamati Maalum ya Kuchunguza Biashara ya Almasi wakiongozwa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mussa Azzan Zungu katika tukio lililofanyika leo katika Viwanja vya Bunge Mjini Dodoma.

IMGL2795

Spika wa Bunge, Job Ndugai (wa pili kulia waliokaa), Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa (wa pili kushoto waliokaa), Naibu Spika wa Bunge, Mhe. Dkt. Tulia Ackson (kushoto waliokaa) na Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Mhe. Freeman Mbowe (kulia waliokaa) wakiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Kamati Maalum ya Kuchunguza Biashara ya Tanzanite wakiongozwa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Dotto Biteko katika tukio lililofanyika leo katika Viwanja vya Bunge Mjini Dodoma.

IMGL2815

Spika wa Bunge, Job Ndugai (wa pili kulia waliokaa),Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa (wa pili kushoto waliokaa), Naibu Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson (kushoto waliokaa) na Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe (kulia waliokaa) wakiwa katika picha ya pamoja na Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya kupokea Taarifa ya Kamati Maalum ya Kuchunguza Biashara ya Almasi na Tanzanite katika tukio lililofanyika leo katika Viwanja vya Bunge Mjini Dodoma.

Kim kardashian kuongeza mtoto wa tatu kwa gharama kubwa
Mbappe: Nilitamani kujiunga na Arsenal