Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars leo imesafiri kuwafuata wapinzani wao Libya mchezo wao wa pili wa kufuzu michuano ya Afcon inayotarajiwa kufanyika nchini Cameroon 2021.
Sars itamenyana na Libya nchini Tunisia ikiwa na kumbukumbu ya ushindi mnono wa mabao 2-1 dhidi ya Equatorial Guinea mchezo uliochezwa jana uwanja wa Taifa.
Kwenye msafara huo nyota Erasto Nyoni ambaye ni kiraka ameachwa nchini kwaajili ya matibabu ya goti.
Etienne Ndayiragije, Kocha Mkuu wa Stars amesema kuwa ameachwa Nyoni kutokana na maumivu ya goti aliyoyapata jana kwenye mchezo dhidi ya Equatorial Guinea.
Stars imeanza vyema michuano ya Afcon kwa kuibuka kidedea mbele ya timu ya Equatorial Guinea kwa kupata ushindi huo ambapo mchezo uliochezwa uwanja wa Taifa.