Na pius yalula-Dar24

Tanzania Mwenyeji maadhimisho ya 6 ya wiki ya Maji Barani Afrika na Mkutano wa 10 wa Baraza la Mawaziri wa Maji wa  Nchi za Afrika yatakayofanyika  Julai,2016 Jijini Dar es salaam.

Kauli hiyo imetolewa na  Mkurugenzi Msaidizi Maji Shirikishi kutoka Wizara ya Maji na Umwagiliaji Bw. Sylivester Matemu wakati wa mkutano na waandishi wa  Habari leo jijini Dar es salaam.

Mgeni Rasmi katika Ufunguzi wa Maonyesho ya Wiki ya maji yatakayofanyika kabla ya mkutano wa Baraza la Mawaziri atakuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa  Kassim Majaliwa.

Akifafanua Matemu amesema kuwa mkutano huo utahusisha washiriki zaidi ya 1000 kutoka mataifa 54 kutoka Bara  la Afrika na wengine kutoka nje ya Afrika.

Maadhimisho  hayo yataambatana na maonyesho ya shughuli za wadau wa sekta ya maji na umwagiliaji, kwenye Ukumbi wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere Jijini Dar es salaam.

Kauli mbiu ya kongomanao hilo ni “ Kufikia lengo la maendeleo Endelevu Juu ya usalama wa Maji na usafi wa mazingira” alibainisha Matemu.

Mkutano huo utawasaidia wataalamu wa maji  kutoka Mataifa mbalimbali ya Afrika kujadiliana kuhusu mikakati mbalimbali itakayosaidia kupambana na changamoto zinazoikabili sekta ya maji katika bara la Afrika.

Akizungumzia faida za Mkutano huo Matemu amesema kuwa  utasaidia kufungua fursa mbalimbali zilizopo katika sekta ya maji na Sekta nyingine ikiwemo kukuza na Kutangaza vivutio vilivyopo hapa nchini hali itakayosaidia kukuza Utalii.

Video: Tume ya haki za binadamu na utawala bora imetoa mapendekezo yake 9 kuhusu haki za Watoto
Barnaba awakacha ‘ma-dancer’