Usiku wa kuamkia leo, Sara Kibonde ambaye ni mke wa mtangazaji wa Clouds FM wa kipindi cha jahazi, Ephraim Kibonde amefariki dunia katika hospitali ya Hindu Mandal alikokuwa akifanyiwa matibabu.

Taarifa kamili juu ya chanzo kilichosababisha mauti kumfika bado hazijawekwa bayana.

Aidha tunapenda kutoa pole kwa familia ndugu jamaa na marafiki wa Sara Kibonde aliyeaga dunia Usiku wa jana Jumanne, Julai 10, 2018.

Mungu ampuzishe kwa amani.

 

Askari ajiua kwa risasi akielekea lindoni
Riyad Mahrez aahidi mazito Man City