Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), yashusha gharama za kupiga simu kutoka shilingi 26.96 kwa dakika moja hadi shilingi 15.60 kuanzia 2018.

Mkurugenzi wa TCRA James Kaliba amesema kuwa gharama hizo zitaendelea kupungua kadiri miaka inavyozidi kwenda kama ambavyo imeanishwa hapa.

Gharama za mwingiliano zitakazotozwa kwa dakika na mwaka kwenye mabano ni Sh15.60 (Januari Mosi, 2018), Sh10.40 (2019), Sh5.20 (2020), Sh2.60 (2021) na Sh2.00 (2022).

Viwango hivyo vimepungua kulinganisha na miaka mitano iliyopita ambayo gharama zake za mwingiliano zilizokuwa zikitozwa kwa dakika na mwaka wake kwenye mabano ilikuwa Sh34.92 (2013), Sh32.40 (2014), 30.58 (2015), Sh28.57 (2016) na Sh26.96 (2017).

Hata hivyo amesema kuwa kampuni za simu zimekuwa na kigugumizi kukubaliana na viwango hivyo na kuingia mikataba ya mwingiliano kwa sababu ya masilahi ya kibiashara hivyo TCRA ililazimika kuingilia kati na kuvipangia kwa kufuata utaratibu kama ilivyoainishwa katika sheria namba 12 ya kuanzishwa kwake mwaka 2003.

“Kupungua kwa gharama hizi kutawezesha na kuongeza ufanisi katika shughuli za sekta zingine kiuchumi na kijamii, pia kutaongeza mapato ya watoa huduma na Serikali kutokana na ongezeko la matumizi ya huduma za mawasiliano,” alisema.

Alisema kwa sasa simu za mezani ni 127,976 na watumiaji wa simu za kiganjani imeongezeka kutoka laini 2,963,737 mwaka 2005 hadi kufikia laini 40,002,364, Septemba na mpaka kufikia Septemba, mwaka huu watumiaji wa huduma wamefikia 21,611,855

Kauli ya Kakobe yamtia mikononi mwa TRA
Video: Vanessa aanika alivyovuta ‘Pumzi ya Mwisho’ kwenye misukosuko