Rais wa La Liga, Javier Tebas amesema kuwa anatamani kumuona tena nyota wa Klabu ya Paris Saint Germain ya Ufaransa, Neymar jr akicheza ligi kuu ya Hispania.

Ameyasema hayo wakati wa sherehe za utoaji tuzo za waandishi wa habari za michezo nchini humo, ambapo amesema kuwa Neymar ni mchezaji mwenye kiwango cha juu na anastahili kurudi nchini Hispania.

”Neymar ni mchezaji mkubwa, natamani nimuone tena akicheza La Liga ila kuhusu timu atakayocheza sitaki kujua,”amesema Tebas

Aidha, Neymar ambaye alisajiliwa na PSG kutoka Barcelona Juni 2017 hadi sasa amefanikiwa kufunga mabao 26 kwenye mechi 24 alizoichezea timu hiyo.

Hata hivyo, bosi huyo wa La Liga amewahakikishia wanahabari kuwa msimu ujao wa ligi 2018/19 hakutakuwa na matatizo ya uamzi kwenye baadhi ya matukio kwasababu teknolojia ya VAR itaanza kutumika nchini humo.

 

Mfaransa wa Simba abebeshwa zigo zito
Almanusura Yanga wang’olewe kombe la shirikisho