Kampuni ya Huawei inasema teknolojia yake ya 5G na kamera za kisasa zitaongeza ufuatiliaji wa wanyama pori katika makazi yao ya asili katika eneo la Afrika, Kusini mwa Sahara, na katika nchi ambazo ziko nyuma kiteknolojia kwa kuongezea, zana za kidijitali za Huawei ambazo zitasaidia kunasa na kusambaza picha za ubora wa juu, za wakati halisi za wanyama, ili kuepusha hatari inayoweza kutokea mbali na kuendeleza utalii barani Afrika.

Lauren Arthur, mhifadhi wa Afrika Kusini na mtangazaji wa televisheni ya wanyamapori alipongeza kutumwa kwa teknolojia ya 5G ya Huawei, akisema italeta mapinduzi makubwa katika ulinzi wa viumbe walio katika hatari ya kutoweka.

Amebainisha kuwa dubu wa Afrika aliye hatarini kutoweka anayeishi Boulders Beach huko Cape Town, Afrika Kusini, amenufaika na mipango ya uhifadhi inayoendeshwa na teknolojia.

Aliongeza kwamba teknolojia ya 5G imekuwa muhimu katika kusaidia wahifadhi kufuatilia makundi ya wanyama katika bara zima la Afrika, na kuongeza kuwa matumizi ya kamera ya 5G itasaidia walinzi kuangalia wanyama wa porini kwa karibu na kuzuia matukio mabaya kama mashambulizi ya nyuki.

“Katika siku zijazo, 5G sio tu itaboresha maisha ya kidijitali ya watu lakini pia italeta manufaa na mabadiliko ya kweli kwa binadamu, makampuni, jamii na mazingira ya asili,” alisema Arthur.

Kando na kutoa zana za kidijitali ili kuimarisha uhifadhi wa viumbe barani Afrika, Huawei pia imesaidia ulinzi ulioimarishwa wa misitu ya mvua kupitia matumizi ya Ufuatiliaji wake wa Kimsingi wa anga.

Huawei imechukua hatua hii baada ya ripoti mbalimbali za hatari kwa wanyapori barani Afrika, Kwa mfano, ripoti muhimu ya Shirika la uhifadhi wa wanyama pori WWF ya mwaka wa 2020, inayosema idadi ya wanyama pori imepungua kwa zaidi ya theluthi mbili katika kipindi kisichopungua miaka 50.

Ripoti hiyo inasema kushuka kwa idadi hiyo hakuoneshi ishara za kupungua, bali imetahadharisha kuwa mazingira ya asili yanaharibiwa na binadamu kwa kiwango ambacho hakijawahi kuonekana awali.

Kwa mujibu wa, afisa mkuu mtendaji katika WWF Tanya Steele, wanyama pori wanapungua kwa sababu ya uchomaji wa miti, kuvua samaki kupita kiasi, na kufanya uharibifu katika maeneo ambayo wanyama pori wanaishi.

Ripoti hiyo imeangazia aina tofauti za wanyama wanaochunguzwa na wanasayansi wa uhifadhi katika maeneo wanaoishi kote duniani.

Walirekodi upungufu wa wastani wa asilimia 68 katika zaidi ya wanyama 20,000 wanaoishi porini, ndege, wanyama wanaoishi ardhini na majini, wanyama wa kutambaa na samaki tangu 1970.

Kwenye orodha ya nchi za Afrika zenye ndovu wengi zaidi, Tanzania ni ya 3 ikufuatiwa na Kenya baada ya Zimbabwe, Botswana.

Rais wa Burkina Faso, Roch Kaboré, azuiliwa na waasi.
Marafiki wa DJ aliyejiua kwa sumu wafunguka chanzo