Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limepinga kitendo cha makampuni mbalimbali kuchezesha michezo ya bahati nasibu (betting) kwa mashindano yanayoandaliwa na Shirikisho hilo.

Taarifa ya Shirikisho hilo iliyotolewa na Afisa Habari na Mawasiliano wa TFF, Baraka Kizuguto imeeleza pia hatua zilizochukuliwa dhidi ya makampuni yanayojihusisha na uchezeshaji bahati nasibu hizo.

Hii ni taarifa ya TFF kwa umma kuhusu Bahati Nasibu: 

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limepokea kwa mshtuko taarifa za kuwepo makundi ya watu na makampuni wanaochezesha michezo ya kubahatisha inayohusu mashindano mbalimbali yanayoandaliwa na kusimamiwa na TFF (betting).

TFF inauthibitishia umma wa watanzania kuwa Shirikisho halihusiki wala halijawahi kutoa kibali chochote cha kuhusisha mashindano yake na michezo ya kubahatisha.

Kwa kuwa baadhi ya wahusika wa matendo hayo ni makampuni ya nje ya nchi hivyo TFF imechukua hatua zifuatazo:

1.TFF imeandika barua kwenye Shirika la Bahati Nasibu ya Taifa ili kupata mwongozo wa kisera na kisheria kuhusu haki na majukumu ya Shirika hilo katika kudhibiti na kusimamia jambo hilo.

2.TFF imeandika barua kwa kitengo cha sheria cha FIFA ili kupata mwongozo na ushauri wa namna ya kudhibiti makampuni ya nje yanayoshiriki mchezo huu.

TFF inawaomba wadau wa mpira wa miguu na washiriki wa michezo ya kubahatisha wajiepushe kushiriki michezo ya kubahatisha inayohushu michezo yote inayoandaliwa na TFF.

TCRA yadai 'Zigo Remix' ya AY imevunja Rekodi Ofisini Kwao, 'inapendwa'
Maalim Seif arejea kutoka India, arusha jiwe la kwanza kwa Polisi