Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF), Jamal Malinzi ametuma salam za pongezi kwa katibu mkuu wa TOC nchini Filbert Bayi kwa kuchaguliwa kuwa Mjumbe wa Kamati ya Ufundi ya Shirikisho la Riadha Duniani (IAAF).

Katika salam zake Malinzi amempongeza Bayi kwa kuchaguliwa katika nafasi hiyo muhimu ya kutunga na kupitisha sheria zinazotumika katika michezo ya Olimpiki Duniani.

Bayi amechaguliwa katika nafasi hiyo ya Mjumbe wa Kamati ya Ufundi ya Olimpiki dunanI katika uchaguzi uliofanyika nchini China, ambapo ataitumikia nafasi hiyo kwa kipindi cha miaka minne.

Kwa niaba ya famili ya mpira wa miguu nchini, TFF inamtakia kila la kheri FIilbert Bayi katika nafasi hiyo aliyochaguliwa na kuahidi kuendelea kushirkiana nae katika kuendeleza michezo nchini.

Udhamini Wazidi Kumiminika Soka La Bongo
Bodi Ya Ligi Yaanika Hadharani Ratiba Ya FDL