Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) limevitaka vilabu vyote nchini vya Ligi Kuu (Vodacom), Ligi Daraja la Kwanza (StarTimes), na Ligi Daraja la Pili (SDL) kuheshimu utaratibu uliowekwa wa usajili na utekelezaji wake, kwani TFF haitapendelea klabu yoyote katika suala hilo.

TFF inachukua fursa hii kuwakumbusha viongozi wote wa vilabu kuhusu kalenda ya mwaka ya usajili ambayo ina vipindi viwili,

(i)  Dirisha Kubwa la Usajili  (Juni 15 – Agosti 20)

(ii)  Dirisha Dogo la Usajili (Novemba 15 – Disemba 15)

Baada ya usajili hufuatia kipindi cha pingamizi ambacho kuchukua wiki moja, kisha Kamati ya Sheria na Hadhi za wachezaji ya TFF kupitia mapingamizi hayo na kupitisha usajili wa wachezaji wote waliosajiliwa.

Kipindi cha usajili wa dirisha dogo ulifunguliwa Novemba 15 na utafungwa kesho Disemba 15, kipindi hichi hutumika kwa ajili ya uhamisho, kutangaza wachezaji wanaoachwa kwa mujibu wa kanuni, kutangaza wachezaji waliositishiwa mikataba, na kipindi cha pingamizi Disemba 16 – 22, na kuthibitisha usajili Disemba 23, mwaka huu.

TFF inaviomba vilabu kufuata utaratibu uliopo kikanuni katika shughuli za uendeshaji wa mpira wa miguu nchini.

Kasi Ya Magufuli Yampitia ‘Dk. Mwaka’, Atimua Mbio, Atakiwa Kujisalimisha
EUROPA LEAGUE: Man Utd Wapangiwa Vibonde, Liverpool Na Spurs Wakwaa Visiki