Kwa mara ya kwanza tangu kuasisiwa kwa ligi kuu ya Uingereza ,thamani ya uuzaji na malipo ya wachezaji,umegonga pauni bilioni moja.

Pauni milioni £965m zilitumika msimu uliopita wa mwaka wa 2014-15,

Huku zikisalia saa chache kabla ya dirisha la uhamisho wa wachezaji katika ligi kuu ya Premia ya Uingereza rekodi mpya imeshawekwa.

Vilabu 20 vya ligi ya premia vimetumia takriban pauni milioni £130 kuanzia Januari mosi-31.

Newcastle imewanunua Jonjo Shelvey, Andros Townsend na Henri Saivet.

Vilevile timu hiyo imeweka dau ya paundi milioni £21m kwa ajili ya kununua huduma za mshambulizi wa West Brom Saido Berahino.

Afsa mmoja wa kampuni ya urasimu ya Sports Business Group at Deloitte, Dan Jones, amesema kuwa ” kwa mara nyengine tumeshuhudia vilabu vinavyoshiriki ligi kuu ya uingereza vikiwekeza kiasi kikubwa mno cha fedha ilikusajili ufundi na huduma za wachezaji.”

“Hii ndio mara ya kwanza kwa thamani ya uhamisho kuzidi pauni bilioni moja”

Mke wa Kafulila aibuka na ununuzi wa Mabehewa Mabovu Bungeni, Mwakyembe aweka rehani ubunge wake
China yatoa onyo kali kwa Marekani kwa kusogeza meli ya kivita kwao