Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la soka nchini  (TFF) litapandisha idadi ya timu zinazoshiriki Ligi Kuu msimu ujao wa 2018/19 kutoka 16 za sasa hadi 20, imefahamika.

Uamuzi huo umefanyika Jumanne Agosti 22, 2017 wakati Kamati ya Utendaji inafanya marekebisho ya Kanuni za Ligi Daraja la Kwanza inayotarajiwa kuanza Septemba 16, mwaka huu.

Kwa marekebisho hayo, timu zitakazoshuka daraja msimu ujao kutoka Ligi Kuu ya Vodacom ya sasa ni mbili hivyo kubaki 14. Na ili kufikia timu 20, timu sita (6) za Ligi Daraja la Kwanza zitapanda daraja.

Kwa mujibu wa utaratibu wa Ligi Daraja la Kwanza, timu, ina maana kwamba msimu huu timu mbili zitapanda kutoka katika kila kundi katika ligi hiyo ambayo inatarajiwa kuanza Septemba 16, mwaka huu.

Makundi ya Daraja, kundi ‘A’ lina timu za African Lyon, Ashanti United, Friends Rangers za Dar es Salaam, JKT Ruvu na Kiluvya United za Pwani, Mgambo JKT ya Tanga, Mvuvumwa ya Kigoma na Polisi Moro ya Morogoro.

Kundi ‘B’ ziko za Coastal Union ya Tanga; JKT Mlale ya Ruvuma; KMC ya Dar es Salam, Mawezi Market ya Morogoro, Mbeya Kwanza ya Mbeya, Mufundi United ya Iringa, Mshikamano na Polisi Dar za Dar es Salaam.

Kundi ‘C’ lina timu za Alliance School, Pamba na Toto

African za Mwanza, Rihno Rangers ya  Tabora, Polisi Mara ya Mara, Polisi Dodoma ya Dodoma, Transit Camp ya Shinyanga na JKT Oljoro ya Arusha.

Rais Karia Amteua Nyamlani, Mgoyi
Watanzania 2 kutua Man City kwa majaribio, Mwakyembe atoa baraka zake