Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA), imetoa tahadhari ya mvua kubwa inayotarajiwa kunyesha Machi 2 – 3, 2020, katika Mikoa ya Mara, Simiyu, Arusha, Kilimanjaro, Manyara, Singida, Dodoma, Kaskazini mwa Mkoa wa Morogoro, Tanga, Dar es Salaam, Pwani pamoja na Visiwa vya Mafia,Unguja na Pemba.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mamlaka hiyo pia imeeleza kuwa mvua hizo pia zitanyesha Machi 4 kwa baadhi ya maeneo ya Mikoa ya Njombe, Iringa, Arusha, Kilimanjaro,Manyara, Dodoma, Tanga, Morogoro, Dares Salaam, Pwani pamoja na Visiwa vya Mafia, Unguja na Pemba.

Mvua hizo zinatarajiwa kunyesha kwa siku tatu mfululizo kuanzia leo Machi 2 hadi Jumatano ya Machi 4, 2020.

TMA pia imeeleza athari ambazo zinaweza kujitokeza kuwa ni pamoja na baadhi ya makazi kuzungukwa na maji, ucheleweshwaji wa usafiri, kusimama kwa muda kwa baadhi ya shughuli za kiuchumi na kijamii na kuwataka wananchi kuzingatia na wajiandae.

 

 

Mkutano wa Baraza la Mawaziri wa SADC Kufanyika nchini Machi 16-17
Stendi ya mkoa Mbezi yabakiza miezi 4 kukamilika, wakandarasi waonywa