Treni mbili, moja ya mizigo na nyingine ya abiria leo zimegongana Kaskazini mwa Misri na kusababisha vifo vya watu 15.

Kwa mujibu wa wizara ya afya ya Misri, mbali na vifo hivyo, ajali hiyo iliyoweka historia ya ajali kwa njia ya reli katika eneo hilo la jimbo la Behaira ilisababisha watu wengine kumi na tano kujeruhiwa vibaya.

Kipande cha video inayoonesha tukio hilo kilichorushwa kwenye televisheni ya taifa kimeonesha wananchi wakisaidiana na kitengo cha wizara ya afya kuwaondoa majeruhi na kuwaweka kwenye magari ya wagonjwa (ambulances).

Afisa wa Wizara ya afya, Alaa Othman aliiambia televisheni ya taifa kuwa majeruhi walikimbizwa hospitalini kwa ajili ya matibabu na kwamba miili yote ya marehemu iliondolewa kwenye eneo la tukio.

Sababu ya ajali hiyo bado haijafahamika. Tukio hilo limetokea ikiwa ni miezi saba imepita tangu watu 41 wapoteze maisha baada ya treni mbili kugongana katika jiji la Alexandria.

Video: Heche aapa kula sahani moja na Musiba
Nyika: Chirwa haendi Simba hata kwa dawa