Rais Mteule wa Marekani Donald Trump anatarajiwa kumteua mkwe wake Jared Kushner, kuwa Mshauri mwandamizi wa Ikulu wa nchi hiyo.

Aidha, Kushner mwenye umri wa miaka 35 ambaye amemuoa binti mkubwa wa Trump, Ivanka ambaye alifanya kazi kubwa wakati wa kampeni za uchaguzi, zilizomuwezesha Trump kushinda.

Majukumu ya kazi yake yanatarajiwa kuhusika na masuala ya sera za nje na ndani ya nchi, ikiwemo masuala ya biashara na Mashariki ya Kati.

Hata hivyo baadhi ya wachambuzi wanahoji kama uteuzi huo utakiuka sheria ya kupinga upendeleo wa undugu katika ajira.

Jared Kushner hata chukua mshahara kwa uteuzi huo wa Ikulu ya Marekani na itampa nafasi ya kumfanya kuwa huru na maslahi ya shughuli zake za kibiashara.

Mghwira awanyooshea kidole wataalamu wa kilimo
FA Cup: Ratiba Ya Mzunguuko Wanne Yatolewa