Katika kuongeza morali na kuwazawadia wachezaji wanaofanya vizuri, Klabu ya Simba ilianzisha Tunzo ya Mchezaji Bora wa Mwezi kuanzia mwezi wa Septemba 2015.

Mshindi wa mwezi wa Oktoba, 2015 ni Mohamed Hussen Tshabalala ambapo alipigiwa kura nyingi na  mashabiki na wapenzi wa Simba na soka la Tanzania kwa ujumla kupitia simu za mkononi ambao pia wamejiunga na huduma ya Simba News.

Akizungumza leo jijini Dar es salaam Rais wa Simba Evans Aveva alisema “Uongozi, wanachama na wapenzi wa Simba wanathamini mno mchango wa wachezaji katika kuifanya timu yetu ifanye vizuri, hivyo ni jambo la busara kama klabu ya kwanza Nchini Tanzania kuwa na tunzo za mchezaji wake bora kuendeleza utamaduni huu tuliokwisha uanza mwezi uliopita ambapo mchezaji Hamis Kizza ndio alishinda tunzo ya mchezaji bora kwa mwezi Septemba. Tunaamini kuwa Tunzo ya Mchezaji bora kwa Mohamed Tshabalala itakuwa chachu ya maendeleo katika kuendelea kucheza soka lake vizuri kwa maendeleo ya klabu na maendeleo yake binafsi katika soka”.

Akizungumza jinsi tuzo ya mchezaji bora itakavyoendeshwa, Mkurugenzi Mkuu wa EAG Group ambao ni washauri na watekelezaji wa Masoko na Biashara wa Simba, Imani Kajula alisema “Wanachama na wapenzi wa Simba na wapenda michezo ndio watakao kuwa wanachagua mchezaji bora wa mwezi kwa kutuma jina la mchezaji wanayempendekeza kwenda kwenye namba 15460, Ni wale tu ambao wamejiunga na Simba News kupitia mtandao wa Voda na Tigo wataweza kupiga kura kuchagua mchezaji bora wa mwezi wa Simba’’

Simba News ni huduma iliyoanzishwa na Simba ili kuwapa wapenzi wa Simba habari mbalimbali za Simba popote pale walipo ikiwemo matokeo, majina ya wachezaji wanaocheza mechi, usajili na habari nyingine za klabu ya Simba. Kujiunga na Simba News tuma neno Simba kwenda namba 15460 ni maalum kwa Tigo na Vodacom.

NEC Yaingilia Kati Ushawishi Kwa Rais Kuhusu Baraza La Mawaziri
Mpambe wa Karibu Wa Lowassa Akutwa na Hili Mikononi Mwa Polisi