Usiku wa Agosti 20 mwaka huu, iliweka historia nyingine kwenye utoaji wa Tuzo za Video za Muziki za MTV (MTV – VMAs) zilizofanyika New York nchini Marekani.

Wasanii wa kike walionekana kutawala tuzo hizo jana, wakizoa tuzo kubwa zaidi kama video bora ya mwaka na msanii bora wa mwaka (Camila), Video ya Wimbo bora wa Hip Hop (Nicki Minaj), Msanii Bora Mpya (Cardi B).

Katika tuzo hizo, Cardi B alikuwa anaongoza kwa kutajwa kwenye vipengele 10 akiwa nyuma ya Jay Z na Beyonce ambao walikuwa wametajwa kwenye vipengele 8 na Drake kwenye vipengele 7.

Tumekuandalia orodha ya washindi wa tuzo hizo kwenye vipengele muhimu.

Video ya Mwaka

Camila Cabello ft. Young Thug – “Havana” – Syco Music/Epic Records

Camila Cabello

Msanii Bora wa Mwaka

Camila Cabello

Wimbo Bora wa Mwaka

Post Malone ft. 21 Savage – “rockstar”

Msanii Bora Mpya

Cardi B

Ushirikiano Bora

Jennifer Lopez Feat. DJ Khaled na Cardi B – “Dinero”

Wimbo Bora wa Pop

Ariana Grande – “No Tears Left to Cry”

Wimbo Bora wa Asili ya Kilatini

J Balvin, Willy William — “Mi Gente”

Wimbo Bora wa Hip-Hop

Nicki Minaj – “Chun-Li”

Video Bora yenye Ujumbe

Childish Gambino – “This Is America”

Video yenye Uongozaji Bora

Childish Gambino – “This Is America”

Video yenye uchezaji bora (Choreography)

Childish Gambino – “This Is America”

Video Bora Kwa kuhaririwa (edited)

N.E.R.D & Rihanna – “Lemon”

Video Bora ya Msimu wa Kiangazi

Cardi B, Bad Bunny & J Balvin – “I Like It”

 

Video: Mtoto wa Majuto akanusha mama yake kutimuliwa 'ameenda matembezi Dar es salaam'
Watu zaidi ya Milioni 1 wakimbia mafuriko India