Ubalozi wa Uingereza nchini, umemtangaza  Diamond Platinumz kuwa balozi wa vijana wa Tanzania, kwa ajili ya mradi unaoangazia kutengeneza kizazi bora kijacho (next generation).
Uteuzi huo umetangazwa na Balozi wa Uingereza nchini, Dianna Melrose kupitia mtandao wa Twitter.
Superstar Diamond @diamondplatnumz is now #Tanzania Youth Ambassador @nextgentanzania @UKinTanzania @VelavanG pic.twitter.com/LznajpM8Z8
— Dianna Melrose (@DMelroseFCO) July 12, 2016
Ubalozi huo wa Diamond umeunganishwa na ushiriki wake katika mradi wa Next Generation Tanzania.
Kuna uwezekano mkubwa kuwa utendaji kazi wake, ukubwa na ushawishi wa Diamond hasa kwa vijana ni vigezo muhimu vilivyompa shavu hilo.