Uchaguzi wa Kamati ya Uongozi (Management Committee) ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania Bara utafanyika Jumapili Oktoba 15, 2017 jijini Dar es Salaam.

Fomu kwa ajili ya wagombea zitaanza kutolewa Agosti 17, 2017 kwenye ofisi za Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF). Mwisho wa kuchukua na kurudisha fomu kwa wagombea ni saa 10.00 jioni Agosti 23, mwaka huu.

Nafasi zitakazowaniwa ni Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, Wajumbe watatu kuwakilisha klabu za Ligi (PL), Wajumbe wawili wa kuwakilisha klabu za Ligi Daraja la Kwanza (FDL), na Mjumbe mmoja wa kuwakilisha klabu za Ligi Daraja la Pili (SDL).

Ada ya fomu kwa nafasi za Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti ni Sh 200,000 (Shilingi lakini mbili) wakati nafasi nyingine zilizobaki ni Sh 100,000 (Shilingi laki moja).

Uchaguzi utaendeshwa kwa mujibu wa kanuni za Uchaguzi za TFF toleo la 2013.

Wagombea kwa mujibu wa kanuni za uendeshaji wa Bodi ya Ligi Kuu ni marais au wenyeviti wa klabu husika.

Wagombea wanatakiwa kuwa wenyeviti au Marais wa klabu husika.

Nafasi ya Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Ligi Kuu Tanzania inagombewa na klabu za Ligi Kuu pekee.

Kushuhudia Mtanange wa Simba Vs Young Africans Shilingi 7000
Wanachama Wa Simba Kupigwa Msasa Wa Mabadiliko