Nchi ya Uingereza imempongeza Rais John Magufuli kwa utendaji wa serikali yake hususan katika kupambana na ubadhirifu wa mali za umma na ufisadi, kwa siku chache alizokaa madarakani.

Sifa hizo za Uingereza zimewasilishwa leo Ikulu jijini Dar es Salaam na Balozi wa nchi hiyo,, Balozi Dianna Melrose.

Balozi Melrose alieleza kuwa nchi yake imeridhishwa na juhudu za Rais Magufuli katika kulinda fedha za umma na kuahidi kushirikiana naye hususan katika kuimarisha idara ya Mahakama na Intelijensia nchini.

“Tunadhani ameonesha msimamo mkali dhidi ya rushwa na ufisadi, na miongoni mwa mambo ambayo tumezungumza ni namna ya kufanya kazi pamoja katika kupambana na rushwa. Tuna mazungumzo katika kuimarisha mifumo ya kiintelijensi na mahakama,” alisema Balozi Melrose.

Katika hatua nyingine, Rais Magufuli alikutana na rais Mstaafu, Dk. Jakaya Kikwete Ikulu lakini mazumgumzo kati yao hayakuwekwa wazi.

Mugabe agonga chumvi nyingine Kimyakimya
Anna Mghwira apaza sauti kuhusu Mgombea urais wa Zanzibar aliyewasaliti