Hivi karibuni msanii wa nyimbo za Bongo fleva nchini, Naseeb Abdul maarufu duniani kama Diamond Platinumz amekuwa akiingia katika skendo za kuchepuka kimapenzi na baadhi ya mastaa mbalimbali hapa nchini akiwemo Tunda na Wema Sepetu.

Kufuatia matukio hayo mama watoto wa Diamond , Zarinah Hassan ameamua kuchukua uamuzi mgumu alioufanya kwa vitendo zaidi kuliko maneno kama ambavyo imezoeleka na kuacha maswali mengi kwa mashabiki wa wawili hao.

Wengi walitegemea kuona Zari akimlushia vijembe baba watoto wake kama ambavyo imekuwa kipindi cha nyuma Diamond alipopata skendo na Hamissa  Mobeto.

Zari kupitia akaunti yake ya instagram yenye wafuasi milion 3 na zaidi ameamua kumu-unfollow baba watoto wake, Diamond Platinumz kitu ambacho kimezua gumzo mtandaoni.

Ujumbe cha mwisho aliopost Zari kabla ya kuchukua uamuzi huo ulikuwa ni:

”There is no secret in life, whatever your Goals, you can get there if you are willing to work”, akimaanisha,

”Hakuna siri katika maisha, unaweza kufikia malengo ikiwa una nia ya kuyafikia, na kufikia malengo yako unatakiwa kuamua na kuwa tayari”. Alituma post hiyo January 30, 2018, siku ambayo Diamond na Wema Sepetu wakiwa stori kubwa ya siku baada ya kuonekana klabu pamoja.

Hayo yamejiri siku chache zilizopita wakati wa uzinduzi wa kumtambulisha rasmi Maromboso katika familia ya WCB, Wema Sepetu akiwa kama mgeni mwalikwa katika shughuli hiyo.

 

 

Marubani 2 wafariki dunia baada ya kulipukiwa na ndege
JPM amlilia Mzee Kingunge