Watu wengi husikika wakisema mapenzi matamu endapo wahusika wanapendana lakini pia ni shubiri pale ambapo hugeuka na kuwa tofauti na matarajio. Maisha ya mahusiano ni maisha ambayo kila kijana anaepevuka lazima atahitaji kuingia au kujaribu kujihusisha.
Watu wengi wanao ingia kwenye mahusiano huwa hawapendi kukubali matokeo yanayotokea mara nyingi pale mambo yanapoenda ndivyo sivyo kwa kudhani kwamba hawakustahili kufanyiwa hivyo au kuona nafsi zao zinadhulumiwa,  Laa hasha!!! Ipo sababu ya wewe kuendelea.
Wakati mambo yanapokuzidia na usipojifunza kuacha yaende kuna uwezekano mkubwa wa kupunguza utendaji kazi wako unapokuwa ofisini kwa kuwa tu maumivu ya mapenzi yatakuwa yanazunguka katika nafsi na ubongo wako.
Licha ya utendaji wa kazi kuwa hafifu lakini bado nafsi inahitaji kuwa na furaha na pindi furaha inapokosekana kuna uwezekano mkubwa wa kupata maradhi tofauti tofauti wakati mwingine hata maradhi ya moyo, kwa sababu kuna jambo tu kubwa umelishika katika nafsi yako.
Kusema ndio kwenye furaha ni kujifunza kusema hapana kwa mambo na watu ambao wanakupatia mawazo. Huna budi kukubaliana na matokeo ya kumwacha aende zake ili uweze kuanza maisha mapya yenye furaha na amani huku ukiwa na tumaini mumgu atakuletea mwingine mwenye kujali hisia zako na kukupafaraja ya moyo.
.