Mpango wa Mazingira wa Umoja wa Mataifa (UNEP) umeripoti kuwa licha ya makadirio kwamba  “uzalishaji wa kaboni utapungua kwa asilimia 7 mwaka huu kutokana na janga la corona”, joto la Dunia linaelekea kuongezeka kwa zaidi ya digrii 3.

Katika taarifa iliyotolewa na UNEP, imeelezwa kwamba ongezeko la joto linaweza kubaki kwa digrii 2 za Celsius ikiwa nchi zitatimiza ahadi zilizotolewa katika Mkataba wa Hali ya Hewa wa Paris, na kwamba uwekezaji wa mazingira unaozingatia hali ya hewa unapaswa kuongezeka.

Katika taarifa hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa UNEP Inger Andersen alisema, “Wakati 2020 ni moja ya miaka yenye joto zaidi katika kiwango cha rekodi, joto lisiloodhibitiwa, dhoruba na ukame vinaendelea kusababisha maafa.”.

Wiki iliyopita, Shirika la Hali ya Hewa Duniani lilitangaza katika ripoti yake ya kila mwaka ya hali ya hewa kwamba 2020 ilikuwa njiani kuwa mwaka wa joto wa tatu baada ya 2016 na 2019.

Namungo FC: Tumepata barua ya FIFA
KMC FC safarini Morogoro kuikabili Mtibwa Sugar