Kesi inayomkabili Mbunge wa Mbeya Mjini (CHADEMA) Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ na Katibu wa Kanda ya Nyassa, Emmanuel Masonga imeahirishwa baada ya kutokea mabishano makali ya Kisheria Mahakamani kutokana na ushahidi uliotolewa

Uamuzi wa kuahirisha kesi hiyo umetolewa na Hakimu Mkazi wa Mkoa wa Mbeya, Michael Mteite baada ya shahidi namba tano Afande Joramu Magova ambaye ni Mkuu wa Kitengo cha Tehama katika Ofisi ya Upelelezi ya Mkoa kutoa ushahidi wake na kumtaka Hakimu kusikiliza sauti zilizokuwa zimehifadhiwa kwenye kinasa sauti.

Aidha, baada ya kutoa kinasa sauti, kulitokea mabishano ya kisheria baina ya Mawakili wa Jamhuri na wa upande wa utetezi ambapo upande wa Jamhuri walikuwa wanataka sauti zisikilizwe na upande wa utetezi ukipinga.

Kutokana na hali hiyo Hakimu Mkazi wa Mkoa wa Mbeya, Michael Mteite ameahirisha kesi hiyo mpaka siku ya kesho ambapo atatoa uamuzi wa juu ya hilo kama utasikilizwa ushahidi huo wa sauti mbele ya Mahakama au la.

Hata hivyo, Mbunge huyo na Katibu wa CHADEMA Kanda ya Nyassa wanashikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za kuzungumza maneno ya uchochezi na yenye kuleta chuki kati ya Serikali na wananchi.

 

 

Juma Nyoso kupandishwa kizimbani
CAF kuzikagua Simba, Young Africans