Mchezo ulopigwa jana usiku kwenye Uwanja wa Amaan katika kombe la mapinduzi kati ya Yanga na Azam FC, umeingiza mashabiki wengi kuliko hata fainali ya mwaka jana kati ya Simba na Mtibwa Sugar.

Mbali ya rikodi hiyo pia mchezo huo umevunja rikodi ya kuingiza watu wengi kuliko michezo yote iliochezwa hadi sasa kwenye michuano hiyo.

Katika mchezo huo ambapo Azam na Yanga wametoka sare ya kufungana 1-1 umeingiza mashabiki mpaka wengine wamekosa pa kukaa jambo ambalo likapelekea kukaa kwenye Tatan za uwanja huo.

Mchezo mwengine unaotarajiwa kuingiza mashabiki wengi utakaochezwa kesho saa 2:15 usiku kati ya Yanga na Mtibwa Sugar ambapo Yanga anahitaji sare tu ili isonge nusu fainali wakati Mtibwa Sugar watalazimika washinde ndipo asonge mbele hasa ikiwa Azam ataifunga Mafunzo katika mchezo unaotangulia kuchezwa mapema kesho.

Kwasasa mechi wanapokutana Yanga na Azam huwa ya ushindani zaidi na hata kufikia hatua ya wachezaji kutaka kurushiana masumbwi jambo ambalo huwenda ikapelekea kuwa ndio mechi kubwa zaidi Tanzania kuliko hata watakapokutana wapinzani wa Jadi Simba na Yanga.

Uwanja wa Amaan unachukua jumla ya Watazamaji 15,000 ambapo pia ndo uwanja mkuu wa michezo Zanzibar, ukiwemo mpira wa miguu kama ada yake lakini hata riadha na mambo mengine zikiwemo sherehe hasa za Mapinduzi januari 12 kila mwaka.

Michael Carrick Ashangazwa Na uvumi Dhidi Yake
Marcello Lippi Awaponda Guardiola, Mourinho Amkubali Ancelotti