Kamanda wa Polisi kanda Maalum ya Rufiji, Onesmo Lyanga amethibitisha kutokea kwa ajali ya ndege ndogo ya shirika la Tropical, iliyokuwa ikiruka kutoka katika kiwanja cha ndege cha Mafia kuelekea Dar es Salaam.

Kamanda Lyanga amesema ajali hiyo imetokea leo Agosti 6 majira ya saa 4:00 asubuhi, baada kuanguka na kuteketea kwa moto na ilikuwa na abiria  takribani tisa.

”Ndege imepata ajali ilikuwa inaruka uwanja wa Mafia kwenda uwanja wa Julius Nyerere Dar es salaam, ilikuwa na watu 9 lakini mpaka sasa hivi hakuna aliyefariki na kuna majeruhi 6 na ndege yote imeteketea.

Aidha, kamanda amesema kuwa majeruhi wote 6 wamekimbizwa hospitali kwa ajili ya matibabu zaidi na kwamba Jeshi la polisi Mkoani humo linaendelea na uchunguzi ili kubaini chanzo cha ajali hiyo.

Video: Mashabiki wa Simba wachangia Damu mkoani Kagera
Madaktari waelezea 'mtihani' baada ya mtoto wa dereva wa RC-Mara kufariki