Nyota ya Wizkid inaendelea kupenya kwenye masikio ya wasanii wakubwa wa Marekani.
Siku kadhaa baada ya Drake kuamu kufanya remix ya wimbo wake ‘Ojuelegba’, Couple ya mastaa wa muziki ya Alicia Keys na producer Swizz Bitz imeonesha jinsi ilivyokunwa masikio na kipaji cha msanii huyo wa Nigeria.
Mastaa hao wamepost kwenye instagram video mbili zinazowaonesha wakicheza kwa shangwe hits za Star Boy Wizkid, Ojuelegba na Carlo.
“This song makes me happy,” aliandika Alicia Keys.
A video posted by Alicia Keys (@aliciakeys) on
Swizz Beatz pia alipost kipande cha video akicheza kwa mzuka Ojuelegba na kuandika kuwa Wizkid ndio msanii anaemkubali zaidi.