Tayari mwenyekiti wa CCM na Rais Mstaafu, Dkt Jakaya Kikwete amefungua mkutano wa kamati kuu ya CCM kwenye ukumbi wa halmashauri kuu ya Taifa ya CCM mjini Dodoma Julai 21, 2016.
Akifungua mkutano huo Dkt Kikwete ameishukuru kamati kuu ya CCM kwa ushirikiano wao katika kipindi chote cha miaka kumi hali iliyopelekea hadi sasa chama hicho kipo imara.