Msanii wa muziki wa Hip Hop, Darassa anayetamba na ngoma yake inayokwenda kwa jina la ‘Muziki’ ambayo inafanya vizuri kwa sasa, amesema heshima ya nchi nzima haiwezi kuletwa na mtu mmoja, kwani heshima hiyo haiwezi kutosha watu wote, hivyo ni lazima kila mtu afanye kitu ili Tanzania ionekane inawatu wanaoweza kufanya muziki mzuri badala yakukaa na kujivunia nchi, watu na uwezo bila kufanya vitu vizuri.

Darassa amesema mapinduzi hayo ya muziki mzuri ni heshima kwa watu wote na wasanii wote wa Tanzania. Amesema ili kufanya muziki mzuri si wasanii kufanya muziki wa ‘style’ yake ila ni kufanya muziki mzuri utakao wagusa watu wote.

Viongozi CHADEMA washikiliwa na Polisi
Obama awafungashia virago wanadiplomasia wa Urusi