Mwanamitindo Hamisa Mobetto ambaye ameingia kwenye sanaa ya muziki na kuachia ngoma yake aliyoiita ‘Madam Hero’, sasa ameachia video ya wimbo huo ambao umeleta gumzo mtandaoni na kuzua mjadala mzito.

Mjadala huo ni kufuatia muonekano wa video yake kuhusishwa na maisha halisi ya mwanamitindo huyo ya kutokuwa na mahusiano mazuri na familia ya baba mtoto wake Diamond Platnumz.

Mwanzo kabisa wa video hiyo Hamisa ameonekana akifukuzwa nyumbani anapoishi akiwa na mimba pamoja na mtoto.

Tazama video hapo chini, kisha acha maoni yako hapa kwa Hamissa.

Video: 'Producer' wa Tanzania ashushiwa kichapo Kenya
DC Jokate aanzisha kampeni ya tokomeza zero Kisarawe