Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam, Lazaro Mambosasa amesema kuwa hali ya usalama jijini humo kwasasa iko shwari.

Ameyasema hayo mapema hii leo alipokuwa akizungumza na Dar24 Media, ambapo amesema kuwa operesheni zinazofanywa na jeshi hilo Kanda Maalum ya Dar es salaam zimesaidia pakubwa kupunguza matukio ya uhalifu.

“Kwasasa hali ya jiji iko shwari kabisa, operesheni tunazozifanya zimesaidia pakubwa sana kupungua kwa matukio ya uhalifu, hivyo hata wananchi wamekuwa wakituletea taarifa pindi wanapoona kuna tatizo,”amesema Kamanda Mambosasa

 

Simba SC yajiweka njia panda kombe la shirikisho Afrika
Jezi namba 13 yastaafishwa Fiorentina