Askofu wa kanisa la ufufuo na uzima Josephat Gwajima amekamatwa na Polisi wakati akiwasili Tanzania akitokea nje ya nchi jana July 12 2016. Kamanda wa Polisi kanda maalum ya Dar es salaam Simon Sirro ameeleza kuwa Askofu huyo alipofika tu uwanja wa ndege alichukuliwa Jeshi la Polisi na amehojiwa kutokana na kauli yake ya uchochezi aliyoitoa kabla hajasafiri.