Katibu Tawala wa Wilaya ya Kinondoni, Stella Msofe amewataka wahitimu wa mafunzo ya ufundi Cherehani kutoka katika Taasisi ya Mibosco iliyopo Kunduchi jijini Dar es salaam kuutumia vizuri utaalamu walioupata katika taasisi hiyo.

Msofe amwataka wahitimu hao kuunda vikundi ili waweze kupatiwa mikopo bila riba, hivyo amewataka waifanyie kazi fursa hiyo.

“Sasa mmehitimu mafunzo haya, ni wito wangu sasa kwamba mkaufanyie kazi utaalamu huu mlioupata, kile ambacho mmekiomba kwenye risala yenu Manispaa italifanyia kazi,”amesema Msofe

Uganda kuwatambua Wahindi kama kabila
Watunisia kuandamana kupinga ugeni wa Mwana wa mfalme wa Saudi