Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda amekutana na Wakandarasi jijini Dar es salaam Kwa nia ya kutengeneza miundombinu ya jiji hilo hasa sehemu zinazokumbwa na mafuriko ya mara kwa mara.

Ameyasema hayo hii leo jijini Dar es salaam alipokutana na Wakandarasi hao ofisini kwake ambapo amewaagiza wenyeviti wa mitaa kuorodhesha mitaa yote ambayo ni korofi.

Amesema kuwa hatua hiyo itasaidia pakubwa kuondoa tatizo hilo ambalo limekua sugu hasa wakati wa masika ambapo mafuriko yamekua yakitokea mara kwa mara.

Magazeti ya ndani na nje ya Tanzania leo Mei 17, 2018
Mpina acharuka kuhusu vibudu vilivyokamatwa Jijini Dar